Tuesday, November 2, 2010

KUTOKA MAJUUU......HALLOWEN PART

                                         haya baada ya kuona picha tupeane shuleee...hii Hallowen party huwa inahusiana na nini maana naona macelebrity woote waulaya wameisherehekea...bila shaka Lady Gaga alilala hii coz ye kila siku naona anadress kihallowen....lol!!

UNIQUE MODEL KUSAKA WAREMBO?!!

                           
Kampuni ya Unique Entertainment imeandaa shindano la uanamitindo linalojulikana kama Giraffe Unique Model 2010 litakalofanyika Desemba 24 mwaka huu katika hoteli ya Giraffe Ocean View.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mkuu wa Unique Entertainment, Methusaleh Magesse alisema kuwa shindano hilo litajumuisha washiriki ishirini.

Alisema kuwa washiriki hao watapatikana katika mchujo utakaofanyika Novemba 20 mwaka huu katika hoteli ya Giraffe Ocean View.

Aliwataja majaji watakaohusika katika mchujo huo kuwa ni mbunifu maarufu wa mavazi nchini Ally Remptula, mwanamitindo Victoria Martin, Miss Tanzania 2009, Miriam Gerald na mcheza filamu maarufu Steven Kanumba.

Alivitaja vigezo vitakavyotumiaka katika shindano hilo kuwa ni urefu wa futi 5’ 8’-6’, hips 35-37, kiuno 26-29 na kifua 32-35.

Vigezo vingine ni muonekano wa kiuanamitindo, kijiamini na umri 18-25, tabia njema na minato.

Aliwataka wasichana wenye sifa hizo kujitokeza Giraffe Hoteli Novemba 20 kwa ajili ya mchujo kupata washiriki 20 watakaoingia kambini katika hoteli hiyo Desemba mwaka huu.

Monday, November 1, 2010

CHUCHU's BIRTHDAY PARTY

MAUGONJWAA JAMANIII NDO NIMEDATA NAYOOO
                                                 LIUGONJWAA LA  JIMOYOOOOO

             HAHAHHA ILIKUWA SIKU YA HALLOWEN HIVYO ALIAMUA ATOKE KAMA UGLYBETY.....;)



                          MAPAMBO NAYO YALIKUWA NA THEME YA HALLOWEN
                                    WAALIKWA NAO WALITOKA KIHALLOWEN PIA


 MAMBO HAYA YALIFANYIKA ABUDHABI

MSHAURINI

Mambo Shamim,
Kusema kweli nimekua ni mdau mkubwa sana wa blog yako hata nikawa mmoja wa watoaji comments kwa watu mbalimbali wanaoomba msaada kupitia blog yako
Sijajua ushauri wetu huwa unawork namna gani but nimeona nami leo niombe ushauri


Mimi nna miaka 27, sijui msichana sijui mwanamke, sijui nijiite mtu mzima lakini huo ndo umri wangu. Kwa sasanipo Nairobi kwa kazi fulani iliyoniweka huku kwa mwaka mmoja hivi kazi ambayo naimaliza na kurudi TZ next week moja kwa moja


Sasa shida yangu ni kwamba toka niingie Pubety nimekuwa na chunusi mpaka leo,imagine huo umri wangu then nilianza period yangu ya kwanza nikiwa na miaka 15 all this time nimekuwa na chunusi hazijawahi isha


Nimetumia cream za kawaida hizi sijui Princess na Persal kwa muda mrefu but In Vain


Mwaka juzi nikahamia kwenye Carolight mpaka mwa huu January, kusema kweli chunusi haziniishi zaidi ya kunibadilisha rangi ya ngozi, mi ni maji ya kunde


But nilivyofika huku nikaanza kutumia bidhaa za oriflame ambazo kusema kweli zimenirudisha kwenye ngozi yangu but chunusi zipo palepale, but kabla ya hapo niliendaga kwenye clinic fulani hiv pale Kwa Remi wanatoa dawa fulani hivi kama maji nilizitumia kama miezi mitatu hivi niliona naibiwa tu kwani hazikuisha na nilispenda kama laki nne hivi coz dawa zao ni expensive na wanatoa midawa kibao


Ila mpaka sasa natumia Oriflame products sema lakini bado ninazo tu, sina chunusi sana ila madoa ndo magumu kutoka, honestly ukiangalia ngozi yangu ya miguu unaweza usiamini kama usoni nipo na chunusi coz nina miguu softiiii


Nimeshafanya skin test na farbek, hata huku hawa oriflame walinifanyia waniambia kuwa nina mafuta mengi na juzi tu nimepima Agha Khan nimeambiwa nna mafuta mengi




Sasa kusema kweli siogopi itakua shingi ngapi coz nimetumia zaid ya hata sijui milioni ngapi toka nianze kutafuta suluhisho hili bila mafanikio so kama kuna mtu anayejua mahali ambapo kwa kweli nikienda ntapata tiba na kuisha ntashukuru nimechoka mwenzenu nadhani unajua chunusi zinavyofanya mtu kuwa unconfortable especially kama ni mtu wa kisasa


Unaweza angalia kwenye facebook picha zangu ukaona michunusi yangu kweli imenichosha...


mwalimmissie@yahoo.com

 kama kuna mtu anaweza nitumia email kunielekeza but naomba ziwe ni sehemu ambazo kweli ntapata msaada staki chochote chenye SIDE-EFFECT mbaya kama kuchubua


Nitashukuru sana
Keep Rolling Mama...fans wako tunaendelea kukupa support
Thanks

THEA KITCHEN PARTY

inaonesha ilikucha saana...Hongera saana THEA ni mmoja kati ya waigizaji wa kike wanaonikuna katika tasnia hii ya filamu za nyumbani....kila la kheri
nimeguswa na swagga la gloves la mainda

jiugonjwaa lilikuwa la nguvuu
kabinti kadogooo nako kalikuwepoooo
D.I.D.A nae alikuwepooo



MECKYSHA DIVA's RAMSA!!

 Ramsa watoto wa kizanzibar wanaitambua kama Get Together... ambayo washkaji wa Mecky Bongo Star Movie anayewakilisha na kati ya UKerewe.. wakiwemo Kajala. Diana Bilayla, Salama waliamua kumkaribisha mshakaji wao kwa style hii

                                                Hii ilikuwa no moja ya burudaniii


                               
kitu chaaa mtarimbo Doroooo kilipigwa mikato ya kibao kataaa.....ni balaaa











                                              tukapata na kitu cha misosiiii then tukasepaaaa