Tuesday, January 11, 2011

Tangazo la Msiba wa Mwalimu Innocentia Banzi


Familia ya marehemu mwalimu Julius Banzi wa Mafiga Morogoro, inasikitika kuwatangazia msiba wa Mwalimu Innocentia Banzi kilichotokea alfajiri ya tarehe 12/01/2011 Dar-es-salaam-Tanzania.

Marehemu ni mama wa:
Dennis Londo wa Helsinki-Finland; Esther Londo na Walonzi Tatala wa Tampere-Finland;
Michael Gomela wa Reading-United Kingdom; Daniel Mtebe wa Stockholm-Sweden.

Habari za msiba huu ziwafikie wakuu wa shule zote za sekondari Tanzania, walimu na wanafunzi wa Kilakala sekondari, Morogoro sekondari na Masanze sekondari. Pia ziwafikie wanachama wote wa chama cha msalaba mwekundu Tanzania; wanachama wote wa chama cha maskauti Tanzania na wanamichezo wote wa Mkoa wa Morogoro.

Mazishi yanatarajiwa kufanyika Morogoro mara tu watoto wa marehemu watakapowasili.
Wale wote ambao mpo Finland msiba upo:
Lautamiehentie
2B 39 Vantaa (kwa maelezo zaidi piga simu 050 4863508, 040 5892123, 040 3750820)

Tanzania upo nyumbani kwa marehemu Mafiga-Morogoro, na Dar-es-salaam upo Mbezi Luis-njia panda ya kwenda Makabe (ulizia kwa Kunambi) Kwa maelezo zaidi piga simu namba:  +255 732201098, +255 717365676, +255 713233843

 R.I.P MWALIM BANZI ALIKUWA MWALIMU WANGU WA MICHEZO SHULE YA SEKONDARI MOROGORO NA MATRON KATIKA KAMBI YA UMISETA KWA UFUPI NDO ALINIFUNDISHA MICHEZO R.I.P

No comments:

Post a Comment